Discover

Topics

Shule Direct Kids

Shule Direct Kids APK

Shule Direct Kids APK

1.9.34 FreeShule Direct Limited ⇣ Download APK (41.64 MB)

Chemsha bongo ujifunze KUSOMA KUANDIKA na KUHESABU bure!

What's Shule Direct Kids APK?

Shule Direct Kids is a app for Android, It's developed by Shule Direct Limited author.
First released on google play in 3 years ago and latest version released in 1 year ago.
This app has 5.6K download times on Google play
This product is an app in Education category. More infomartion of Shule Direct Kids on google play
Shule Direct Kids ni app iliyobuniwa kwa ajili ya matumizi ya watoto wa shule za msingi nchini Tanzania. App inamsaidia mtoto wa darasa la kwanza hadi la saba, kujifunza na kuongeza umahiri wa kusoma, kuandika na kuhesabu kwa kutumia michezo iliyotengenezwa kutokana na mtaala na muongozo wa elimu ya msingi nchini Tanzania.

Mzazi tumia App hii kupata taarifa ya maendeleo ya mtoto wako pia kumsaidia kuyamudu zaidi masomo yake au yale maeneo yanayompa changamoto. App hii pia inakusaidia mzazi kufahamu mambo yote anayotakiwa kujifunza mtoto wako pindi awapo shuleni.

FAIDA ZA SHULE DIRECT KIDS
- Kupenda kujifunza
- Kujifunza kwa Uhuru, Muda Wowote, Mahali Popote
- Nyenzo zinazofuata mtaala wa Taifa wa Elimu ya Msingi darasa la 1 - 7
- Kujifunza matumizi sahihi na salama ya teknolojia na mifumo yake
- Kumfanya mtoto kuwa mbunifu zaidi
- Kuweka kumbukumbu na taarifa zote za mtoto, kumsaidia mzazi kupata ripoti kwa haraka na kufuatilia kwa karibu
- Kuongeza ufaulu


Pakua Shule Direct Kids App sasa BURE!


KUHUSU SHULE DIRECT
Shule Direct ni shirika lisilo la kiserikali nchini Tanzania lililojikita kwenye matumizi ya teknolojia na mifumo yake katika kuongeza wigo na fursa za upatikanaji wa nyenzo bora za kujifunzia kwa wanafunzi na walimu wa shule za msingi na sekondari ili kuongeza ufaulu na matokeo chanya ya elimu. Tunafanya kazi na walimu bora wanaokidhi vigezo vya ufundishaji, kutengeneza nyenzo za kujifunzia katika mifumo ya notes, chemsha bongo, mafumbo na michezo mbalimbali kwa kufuata mitaala na miongozo ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa elimu ya msingi na sekondari. Nyenzo zetu zinapatikana kwa njia mbalimbali zikiwemo application za simu, mtandao wa www.shuledirect.co.tz mfumo wa offline Learning Management System (LMS) pamoja na njia ya ujumbe mfupi wa maandishi (SMS).

WASILIANA NASI
Kama una swali, maoni, ushauri, au unahitaji msaada au taaria zaidi, wasiliana nasi kupitia [email protected] Tushirikiane kwa mafanikio ya mtoto wa Tanzania.